Home Soka Minyama Yamkwamisha Balinya

Minyama Yamkwamisha Balinya

by Sports Leo
0 comments

Kocha wa Yanga Mwinyi Zahera amesema sababu kubwa ya kutomtumia mshambuliaji wake Juma Balinya katika mchezo wa kimataifa wa kuwania kufuzu hatua ya makundi ya klabu bingwa barani Afrika ni uzito wa mchezaji huyo kuongezeka.

Zahara amesisitiza kuwa mchezaji huyo aliongezeka kilo baada ya kumaliza ligi kuu nchini Uganda hivyo kuwa mzito uwanjani wakati anajiunga na wanajangwani hao.

“Nilimtaka apunguze kilo haraka, nimpongeze kwenye hilo na tatizo ndiyo sababu ya kwanza kumuweka benchi mchezo wetu na Zesco tuliocheza hapa nyumbani licha ya kuwa na mipango ya kutaka kumtumia kwenye mchezo wa marudiano,” amesema Zahera.

banner

Hata hivyo kocha huyo amesisitiza kuwa atamtumia mchezaji huyo kwenye mechi ya marudiano ugenini dhidi ya Zesco mchezo ambao Yanga inatakiwa ishinde au itoe sare kuanzia mabao 2.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited