Home Soka Miraji Akwaa Tuzo Vpl

Miraji Akwaa Tuzo Vpl

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji wa timu ya Simba sc Miraji Athuman ametwaa tuzo ya mchezaji bora wa ligi kuu Tanzania bara kwa mwezi Septemba  akiwashinda Meddie Kagere na Ismail Kada wa Prisons ya Mbeya.

Kwa mujibu wa shirikisho la soka nchini (Tff) Miraji ametwaa tuzo hiyo baada ya kuisadia timu ya Simba kushinda michezo minne ya ligi iliyocheza mpaka sasa huku akifunga mabao mawili na kusaidia upatikanaji wa mabao mengine mawili kwa mwezi  septemba pekee.

Miraji aliisaidia Simba kupata alama tatu mbeli ya Mtibwa Sugar baada ya kushinda 2-1 huku wakishinda 3-0 dhidi ya Kagera sugar na 2-0 dhidi ya Biashara United.

banner

Miraji alikulia akademi ya Simba sc kasha baadae alicheza timu kadhaa ikiwemo Toto Afrika na baadae akaenda Lipuli Fc kisha akasajiliwa Simba ambapo hakutegemewa kufanya vizuri mbele ya mastaa kama Ibrahim Ajib,Deo Kanda na wengine.

Kutokana na tuzo hiyo mchezaji huyo atajipatia fedha Taslimu za kitanzania shilingi milioni moja na kisimbuzi cha Azam Tv.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited