Home Soka Misumari Yamchosha Bigirimana

Misumari Yamchosha Bigirimana

by Dennis Msotwa
0 comments

Kiungo mshambuliaji mpya wa klabu ya Yanga sc Issa Bigirimana amedai halioni lango anapokua anaichezea klabu hiyo kutokana na kupigwa misumari (Kurogwa) na mchezaji mwenzake wa timu hiyo.

Mchezaji huyo aliyesajiliwa kutoka Apr ya nchini Rwanda amefunguka hayo baada ya kushindwa kuonyesha kiwango mazoezini na kutopata nafasi katika michezo mbalimbali ya klabu hiyo huku akiandamwa na majeraha ya nyama za paja.

Bigirimana raia wa Burundi amedai kuna mchezaji wa nafasi ya ushambuliaji amekua akimfanyia vitendo hivyo ili asipate nafasi ya kucheza klabuni hapo.

banner

Kocha Mwiny Zahera hakupatikana alipotafutwa na Sportsleo ili kujibu tuhumu hizo za mambo ya ushirikina kikosini humo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited