Kiungo mshambuliaji mpya wa klabu ya Yanga sc Issa Bigirimana amedai halioni lango anapokua anaichezea klabu hiyo kutokana na kupigwa misumari (Kurogwa) na mchezaji mwenzake wa timu hiyo.
Mchezaji huyo aliyesajiliwa kutoka Apr ya nchini Rwanda amefunguka hayo baada ya kushindwa kuonyesha kiwango mazoezini na kutopata nafasi katika michezo mbalimbali ya klabu hiyo huku akiandamwa na majeraha ya nyama za paja.
Bigirimana raia wa Burundi amedai kuna mchezaji wa nafasi ya ushambuliaji amekua akimfanyia vitendo hivyo ili asipate nafasi ya kucheza klabuni hapo.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Kocha Mwiny Zahera hakupatikana alipotafutwa na Sportsleo ili kujibu tuhumu hizo za mambo ya ushirikina kikosini humo.