Home Soka Mo Afungukia Usajili Simba sc

Mo Afungukia Usajili Simba sc

by Sports Leo
0 comments

Bilionea wa klabu ya Simba sc Mohamed Dewji amewataka wanasimba kuwa watulivu hasa katika kipindi hiki cha usajili kwani watasajili mchezaji yeyote wanayemtaka.

Mo amesema hayo kupitia mtandao wake wa kijamii wa Twitter ambapo alisema mashabiki hao hawana haja ya kuhofia chochote kwani watasajili mchezaji yeyote atakayependekezwa na mwalimu kutoka timu yeyote.

“Wanasimba wenzangu nataka niwahakikishie hakuna mchezaji yeyote atakayeondoka Simba lakini pia tutasajili mchezaji yeyote kutoka mahali popote kama mwalimu wetu atamhitaji,Tutashuka kwa kishindo hatuna maneno mengi lakini tupo”.

banner

Kauli hiyo inaweza kuwa mwiba kwa wapinzani wao Yanga sc ambao wanashindani kuwasajili mastaa kadhaa akiwemp Bakari Mwamnyeto na mastaa wa kigeni.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited