Home Soka Mokoena Anukia Al Ahly

Mokoena Anukia Al Ahly

by Sports Leo
0 comments

Kiungo wa klabu ya Mamelod  Sundowns ya Afrika ya Kusini Teboho Mokoena anatajwa kuwa mbioni kujiunga na mabingwa wa klabu bingwa barani Afrika klabu ya Al ahly ya nchini Misri baada ya mabingwa hao kuvutiwa na kiwango cha kiungo huyo katika michuano ya mataifa ya Afrika inayoendelea nchini Ivory Coast.

Staa huyo kama dili litafanikiwa atajiunga na Al ahly mwishoni mwa msimu na sasa klabu hiyo inajiandaa kutuma ofa rasmi kwa Mamelod juu ya kumnasa staa huyo mzawa nchini Afrika ya kusini ambaye amekua katika kiwango bora kwa sasa.

Mamelod Sundowns wapo tayari kumuuza staa huyo endapo itatokea ofa nono kutoka timu ambazo zinamhitaji staa huyo ambaye alipitia katika akademia ya SuperSports United ya nchini humo huku Mamelod ikimsajili msimu wa 2022/2023 na mpaka sasa ameichezea timu hiyo michezo 42 akifunga mabao 2.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited