Home Soka Morrison Amvaa Manara

Morrison Amvaa Manara

by Sports Leo
0 comments

Winga mwenye vituko wa klabu ya Simba sc Benard Morrison amemvaa msemaji wa klabu ya Yanga sc Haji Manara ambaye alikua anahamasisha mashabiki wa klabu ya Yanga sc kujitokeza kwa wingi uwanja wa ndege wa Jk Nyerere kumpokea staa Koffi Olomide anayewasili kuja kutumbuiza uwanja wa Taifa katika tamasha la wiki ya Mwananchi.

Morrison aliyekua anacheza Yanga sc kabla ya Simba sc kumsajili kimafia kiasi cha Yanga sc kukimbilia mahakama ya michezo ya kimataifa Cas kuhitaji ufumbuzi wa suala hilo,alimvaa Manara kupitia mtandao wa Instagram ambapo msemaji huyo alikua ameposti picha ikiwa na maneno kama inavyoonekana hapo chini.

banner

Komenti hiyo ya Morrison imezua mtafaruku mitandaoni huku wadau wa soka nchini wakisubiri kuona manara atajibu nini maana inafahamika nae ni mtu wa vijembe.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited