Home Soka Mrithi wa Ndayiragije Atambulishwa Azam Fc

Mrithi wa Ndayiragije Atambulishwa Azam Fc

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Azam fc leo imemtambulisha rasmi kocha Aristica Cioaba kama kocha mkuu wa klabu hiyo akichukua nafasi ya Ettiene Ndayiragije ambaye anakwenda kuwa kocha mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania(Taifa stars).

Cioaba aliyewahi kuwa kocha wa timu hiyo miaka miwili iliyopita ametambulishwa rasmi mbele ya waandishi wa habari huku akiahidi kufanya makubwa zaidi.

“Naushukuru uongozi wa Azam FC kwa kuendelea kuwa na imani na mimi, kikubwa mimi sio mgeni hapa naijua timu, wachezaji wananijua na pia wanafahamu falsafa yangu, jambo kubwa ni kuendelea kuifanya timu kuwa juu pamoja na kushinda mataji,” alisema.

banner

Aidha, kama ilivyokuwa awali Cioaba, mwenye leseni ya juu ya ukocha ya UEFA Pro Licence, amerejea sambamba na Kocha wa viungo, Costel Birsan, aliyekuwa naye awali kipindi anaifundisha Azam FC.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited