Klabu ya Azam fc leo imemtambulisha rasmi kocha Aristica Cioaba kama kocha mkuu wa klabu hiyo akichukua nafasi ya Ettiene Ndayiragije ambaye anakwenda kuwa kocha mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania(Taifa stars).
Cioaba aliyewahi kuwa kocha wa timu hiyo miaka miwili iliyopita ametambulishwa rasmi mbele ya waandishi wa habari huku akiahidi kufanya makubwa zaidi.
“Naushukuru uongozi wa Azam FC kwa kuendelea kuwa na imani na mimi, kikubwa mimi sio mgeni hapa naijua timu, wachezaji wananijua na pia wanafahamu falsafa yangu, jambo kubwa ni kuendelea kuifanya timu kuwa juu pamoja na kushinda mataji,” alisema.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Aidha, kama ilivyokuwa awali Cioaba, mwenye leseni ya juu ya ukocha ya UEFA Pro Licence, amerejea sambamba na Kocha wa viungo, Costel Birsan, aliyekuwa naye awali kipindi anaifundisha Azam FC.