Home Soka Mshahara Wa Banda Kufuru Sauzi

Mshahara Wa Banda Kufuru Sauzi

by Sports Leo
0 comments

Soka linalipa ndio kauli ambayo unaweza kuisema kufuatia mchezaji wa kitanzania Abdi Banda kusaini mkataba mnono huko bondeni baada ya kujiunga na timu ya Highland Park inayoshiriki ligi kuu nchini Afrika kusini.

Timu hiyo iliyoanzishwa mwaka 1959 inatumia uwanja wa Balfour Park Stadium unaoingiza watazamaji 13500 imemsaini beki huyo akitokea Baroka Fc ya nchini humo aliyojiunga nayo akitokea Simba sc iliyomsajili kutokea Coastal union ambayo ilimlea tangu akiitumikia timu ya vijana ya klabu hiyo.

Banda amesaini mkataba huo ambapo atakua analipwa randi 150000 ambayo ni takribani ni kiasi cha shilingiza kitanzania milioni 24 kwa mwezi kiasi ambacho ni kingi ikilinganishwa na mishahara wanayolipwa mastaa nchini.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited