Klaby ya Namungo ya Lindi imefanya utalii wa ndani kwa kutembelea hifadhi ya taifa ya Bonde la Ngorongoro iliyopo Jijini Arusha ikiwa ni sehemu ya burudani na kuchangamsha na kuweka akili sawa kueleka msimu mpya ligi kuu soka Bara.
Wauaji hao wa Kusini wameweka kambi ya maandalizi ya msimu mpya wa 2021/2022 katika akademi ya soka ya Black Rhino iliyopo katika Wilaya ya Karatu mkoani Arusha.
Mastaa mbalimbali wa timu hiyo wameonekana wakifurahia ziara hivyo,wachezaji wapya waliosajiliwa katika dirisha la usajili kama David Molinga na Obrey Chirwa walionekana wakichukua picha mbalimbali za ukumbusho hifadhini hapo.
Namungo inatarajia kucheza mchezo wake wa kwanza wa ligi kwa msimu wa 2021/2022 Septemba 27 dhidi ya Geita Gold katika dimba la Ilulu watakalolitumia kipindi ambacho uwanja wake wa nyumbani wa Majaliwa ukiwa katika marekebisho pamoja na ufungaji wa taa.
Â