Home Soka Ndemla Atua Mtibwa Sugar

Ndemla Atua Mtibwa Sugar

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Mtibwa Sugar imemtambulisha rasmi kiungo Said Ndemla iliyemsajili kutoka Simba sc kwa mkataba wa mkopo wa msimu mzima wa ligi kuu wa 2021/2022.

Ndemla aliyekuzwa na klabu ya Simba sc ametolewa kwa mkopo kwa mapendekezo ya mwalimu Didier Gomes ambaye amesajili mastaa kadhaa kutoka baadhi ya timu za ndani na nje ya nchi hivyo hakuona haja ya kubaki na kiungo huyo kipenzi cha mashabiki wa klabu ya Simba sc.

Baadhi ya mastaa wamejiunga na Mtibwa Sugar wakiwemo Abdi Banda hivyo ujio wa Ndemla klabuni hapo utakwenda kuongeza ushindani katika mechi zaligi kuu msimu ujao.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited