Home Soka Ninja Awatema Yanga sc

Ninja Awatema Yanga sc

by Sports Leo
0 comments

Beki Abdallah Shaibu “Ninja”amesaini mkataba na timu ya klabu ya MFK Vyoskov inayoshiriki ligi daraja la tatu Jamhuri ya Czech wa miaka minne na kisha kutolewa kwa mkopo katika timu ya MFK la Galaxy ya Marekani.

Inasemekana beki huyo Mzanzibar tayari ameshasaini mkataba huo na muda wowote ataondoka nchini endapo taratibu za viza zikikamilika na kwenda nchini humo.

Mchezaji huyo ambaye alisajiliwa na Yanga miaka miwili iliyopita alitajwa kuwa mrithi wa nahodha msitaafu Nadir Haroub licha ya kukubwa na changamoto mbalimbali katika msimu wa kwanza ikiwemo kukosa nafasi ya moja kwa moja kikosini.

banner

Inaripotiwa kwamba klabu ya Yanga bado imeendelea na juhudi za kumsaka mlinzi huyo ili kumuongezea mkataba wa kuendelea kukipiga klabuni hapo kama ripoti ya kocha Zahera inavyotaka.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited