Home Soka Niyonzima Kuivaa Kagera Sugar

Niyonzima Kuivaa Kagera Sugar

by Sports Leo
0 comments

Daktari wa klabu ya Yanga, Docta Shecky Mngazija amesema kiungo wa Klabu hiyo Haruna Niyonzina hajaumia Sana hata leo anaweza kuungana na wachezaji wenzake kwa ajili ya mazoezi ya maandalizi ya mchezo dhidi ya Kagera Sugar mchezo ambao utafanyika alhamisi ya July 09.

Niyonzima aliumia katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Biashara United uliofanyika mjini Musoma ambapo alitolewa na nafasi yake kuchukuliwa na Abdulaziz Makame,Mchezo ambao ulimalizika kwa sare.

Kuumia kwa kiungo huyo maestro kumeleta taharuki kuelekea mchezo wa watani wa jadi utakaofanyika Julai 12 jijini Dar es salaam katika mchezo wa nusu fainali kombe la shirikisho.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited