Home Soka Nizar Aahidi Makubwa Yanga sc

Nizar Aahidi Makubwa Yanga sc

by Sports Leo
0 comments

Kocha Msaidizi mpya wa Yanga, Nizar Khalifan amesema amejiunga na timu hiyo kushirikiana na benchi la ufundi linaloongozwa na Kocha Mkuu, Cedric Kaze kuhakikisha miamba hiyo inachukua taji la Ligi Kuu.

Akizungumza baada ya kutambulishwa, Nizar alisema atasaidiana kwa nguvu na akili yake yote na viongozi waliopo kutoa alichonacho kuendeleza dhamira ya klabu hiyo.

“Nimshukuru Mungu kwa kupata nafasi hii, tulikuwa watano tulioomba lakini nimebahatika mimi, tutasaidiana kwa hali na mali kuendeleza dhamira ya Yanga,” alisema.

banner

Nizar aliyekuwa kocha wa timu ya daraja la kwanza ya African Lyon amewahi kuzichezea timu mbalimbali kama Singida United, Pamba, Moro United na Vancouver Whitecaps ya Canada.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited