Home Soka Nyoni,Kennedy Mambo Safi Simba sc

Nyoni,Kennedy Mambo Safi Simba sc

by Sports Leo
0 comments

Baada ya kumalizana na mabeki wa pembeni kwa kuwaongezea mikataba sasa klabu ya Simba sc imemalizana na mabeki wa kati Erasto Nyoni na Kennedy Juma ambao mikataba yao iko mwishino kumalizika.

Inadaiwa tayari makubaliano ya kuongeza mikataba mipya ya mabeki hao imeshafikiwa na kilichobaki ni kukamilisha baadhi ya taratibu ili wasaini mikataba hiyo ili kuendelea kukipiga katika klabu hiyo inayoelekea kutwaa taji la ligi kuu nchini kwa mara ya nne.

Awali zaidi ya mastaa sita walikua mbioni kumaliza mikataba klabuni hapo na hivyo kufanya kuwepo na minong’ono mingi juu ya uzembe wa uongozi kutowapa mikataba wachezaji hao hivyo kufikia makubaliano hayo ni habari njema kwa mashabiki waklabu hiyo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited