Home Soka Okwi Hali Tete Misri

Okwi Hali Tete Misri

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji wa zamani wa timu ya Simba sc Emmanuel Okwi amekumbwa na ukame wa mabao baada ya kucheza mechi tatu za ligi kuu nchini Misri na kushindwa kufunga bao.

Okwi anayeichezea klabu ya Al Ittihad ya nchini humo mpaka sasa amecheza mechi hizo huku mbili akimaliza dakika 90 na moja akicheza kwa dakika 65 lakini hajafunga mpaka sasa kinyume na matarajio ya wengi baada ya kufanya vizuri akiwa nchini.

Okwi alicheza dhidi ya Zamalek na El Gouna kwa dakika zote tisini na hakufunga bao licha ya timu yake kupoteza kwa bao 1-0 huku mechi dhidi ya Al Masry wakishinda kwa bao moja huku wakishika nafasi ya tano kwenye ligi baada ya kuwa na pointi 6 huku Al Ahly wakiongoza ligi kwa pointi 9.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited