Home Soka Paspoti Yamkwamisha Fei Toto Stars

Paspoti Yamkwamisha Fei Toto Stars

by Sports Leo
0 comments

Kiungo wa klabu ya Yanga sc na timu ya taifa ya Tanzania Feisal Salum “Fei toto” ameshindwa kusafiri na timu ya taifa kwenda nchini Rwanda kucheza mchezo wa kirafiki na timu ya taifa ya nchi hiyo(The Amavubi) baada ya kukosa hati ya kusafiria(pasipoti).

Kiungo huyo ameungana na beki Kelvin Yondani ambaye naye ameshindwa kusafiri na timu hiyo baada ya kupata majeraha na hivyo kuwafanya wote kukosa mechi hiyo pamoja na ile ya kuwania kufuzu michuano ya mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani (Chan) dhidi ya Sudan.

Ettiene Ndayiragije ambaye ni kaimu kocha mkuu wa timu ya taifa amethibitisha kukosekana wachezaji hao huku Fei toto akisema pia licha ya tatizo la hati pia anauguliwa na baba yake mzazi.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited