Bao la Paul Pogba dhidi ya Bunley limeipa alama tatu Manchester United na kuifanya ikae juu ya msimamo wa ligi kuu nchini Uingereza.
Man united ilipata bao hilo baada ya Pogba kupokea pasi ya Marcus Rashford na kupiga shuti lililomshinda golikipa na kusababisha Man united kuongoza ligi ikiwa na alama 36 baada ya kucheza michezo 17 huku Liverpool wakishika nafasi ya pili wakiwa na alama 33 huku wakiwa wamecheza michezo sawa na Man utd.