Licha ya kikosi cha Yanga kuwa safarini mkoani Kagera kuwavaa Kagera Sugar imebainika mastaa saba wameachwa jijini Dar es salaam kuwasubiri Mtibwa Sugar watakaovaana nao Septemba 27.
Mastaa hao saba wameachwa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo majeraha pamoja na kukosa nafasi katika kikosi cha kwanza ambapo mastaa kama Abdulaziz Makame,Paulo Godfrey,Abdala Shaibu Ninja,Juma Mahadhi pamoja na Adam Kihondo wakiachwa kutokana na kukosa namba huku Farouk Shikhalo pamoja na Mapinduzi Balama waliachwa kutokana na kukosa nafasi.
Yanga itacheza na Kagera Sugar kesho saa kumi jioni katika uwanja wa Kaitaba mjini Kagera mchezo unaotazamiwa kuwa mkali na wa kusisimua kutokana na ushindani uliopo baina ya pande zote.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.