Home Soka Samatta “Out” Uefa

Samatta “Out” Uefa

by Sports Leo
0 comments

Timu ya Krc Genk anayoichezea Mtanzania Mbwana Samatta imetolewa nje ya michuano ya ligi ya mabingwa barani ulaya baada ya kukubali kipigo cha mabao 4-0 mbele ya Napoli katika mchezo uliofanyika katika uwanja wa San Paulo jijini Napoli.

Mabao ya Napoli yalipatikana dakika za 2,26 na 78 kupitia kwa Arkadiusz Milk aliyefunga hat trick huku bao la nne likipatikana kwa njia ya penati mpigaji akiwa ni Dries Mertens.

Kwa matokeo ya jana ya kundi hilo la E  Liverpool na Napoli wanafuzu hatua ya 16 bora huku Genk na Redbull Salzburg wakiyaaga mashindano japo Salzburg ataingia hatua ya pili ya ligi ya Europa.

banner

Genk wameyaaga mashindano hayo wakiwa hawajashinda hata mchezo mmoja huku Samatta akiweka rekodi ya kufunga mabao matatu katika michuano hiyo mikubwa barani ulaya.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited