Kesho cha Simba kesho alfajiri kikosi kitaondoka jijini Dar es Salaam kwenda mkoani Mtwara ambako Jumapili Julai 5, 2020 kitacheza mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Ndanda FC utakaofanyika katika uwanja wa Nangwanda Sijaona.
Simba sc inaondoka kuelekea Mtwara huku tayari ikiwa imetwaa taji la ligu kuu kwa mara ya tatu mfululizo huku ikitarajiwa kuondoka na kikosi kamili isipokua beki Shomari Kapombe ambaye ni majeruhi huku Kennedy Juma nae akiwa katika hatihati.