Home Soka Simba sc Baba Lao

Simba sc Baba Lao

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc imefanikiwa kuifunga timu ya As Vita 1-0  katika mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi klabu bingwa barani Afrika uliofanyika nchini Congo Drc.

Katika mchezo ambao ulitawaliwa na mbinu kutoka kwa makocha wa pande zote uliamliwa na bao la penati la dakika ya 60 iliyopatikana na ya beki wa As Vita kuunawa mpira ndani ya eneo la hatari na Chriss Mugalu kufunga penati hiyo kwa ustadi mkubwa.

Licha ya mabadiliko yaliyofanywa na kocha Florent Ibenge ya kuwatoa mastaa kadhaa akiwemo Papy Tshitshimbi Simba sc ilifanikiwa kulilinda bao hilo mpaka dakika ya mwisho ya mchezo.

banner

Simba sc inatarajiwa kutua nchini kesho jumapili na itakua na kibarua kingine cha kujiuliza mbele ya mabingwa wa Afrika Al- Ahly katika uwanja wa mkapa februari 23.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited