Home Soka Simba sc Yaweka Mzigo Kwa Mwamnyeto

Simba sc Yaweka Mzigo Kwa Mwamnyeto

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc imewasiliana na meneja wa beki wa klabu ya Yanga sc Bakari Mwamnyeto ili kuweza kumsajili baada ya mkataba wake na klabu ya Yanga sc kuelekea mwishoni ambapo utafikia tamati agosti mwaka huu.

Meneja wa beki huyo anaitwa Kassa Mussa anayeishi nchini Italia kwa sasa tayari amepokea ofa hiyo nono ya klabu ya Simba sc ikitaka kumsajili beki huyo ili akawe mbadala wa beki Serge Pascal Wawa ambaye viongozi wa klabu hiyo wamekubaliana kuachana nae wakiona kuwa umri umemtupa mkono huku beki Joash Onyando nae akiwa hajasaini mkataba mpya mpaka sasa.

Pia licha ya klabu ya Simba sc kuweka ofa hiyo mezani pia ipo klabu ya kutoka nchini Uturuki ambayo pia imeonyesha nia ya kumsajili beki huyo kijana na nahodha wa klabu ya Yanga sc ambayo nayo imeonyesha nia ya kuendelea kuwa nae ikitaka kuongeza mkataba nae huku pia mchezaji mwenyewe akiwapa kipaumbele wanajangwani hao.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited