Home Soka Simba sc Yazoa alama 3 Tanga

Simba sc Yazoa alama 3 Tanga

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc imefanikiwa kuchukua alama tatu katika mchezo muhimu wa ligi kuu dhidi ya Coastal Union uliofanyika jijini Tanga baada ya kuifunga kwa jumla ya magoli 2-1 katika dakika tisini za mchezo.

Ikianza mpira kwa kuwatumia Chris Mugalu,Benard Morrison na Kibu Dennis,Simba sc ilifanikiwa kupata bao dakika ya 39 kwa juhudi binafsi akiuwahi mpira uliomgonga na kumchungulia kipa Musa Mbise na kuandika bao la uongozi lililodumu mpaka mapumziko.

Kipindi cha pili Coastal waliamka na kushambulia kwa kasi na kufanikiwa kupata bao la kusawazisha dakika ya 76 likifungwa na Victor Patrick Akpan ambaye aliuchopu mpira uliojaa nyavuni na kumshinda kipa Aishi Manula lakini Meddie Kagere alisawazisha dakika tatu za nyongeza baada ya tisini kuisha na kuipa alama tatu Simba sc.

banner

Simba sc sasa imefikisha alama 40 ikiwa katika nafasi ya pili ya msimamo na itawavaa Polisi Tanzania siku ya Jumapili ikiwa ni mchezo wa kiporo utakaofanyika mkoani Moshi katika uwanja wa Ushirika.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited