Home Soka Stars Kuagwa leo,Kapombe Out

Stars Kuagwa leo,Kapombe Out

by Dennis Msotwa
0 comments

Timu ya soka ya taifa ya Tanzania(Taifa stars) inatarajiwa kuagwa leo mchana katika kambi ya timu iliyopo katika hoteli ya Whitesand jijini Dar es salaam.

Timu hiyo inatarajiwa kuondoka kesho kuelekea nchini Misri kwa ajili ya maandalizi ya mwisho ya michuano hiyo ambapo itacheza michezo kadhaa ya kirafiki kabla ya kupeperusha karata ya kwanza june 23 mwaka huu dhidi ya Senegal.

Hafla ya kuwaaga wachezaji hao itaongozwa na naibu waziri wa sanaa,tamaduni na michezo Mheshimiwa Juliana Shonza ambaye atawakabidhi bendera ya taifa.

banner

Pia Tff imedhibitisha kuwa mchezaji Shomari Kapombe hatakuwa sehemu ya msafara wa timu hiyo ili kumpa muda zaidi wa matibabu ya majeraha yake aliyopata akiwa na kambi ya timu ya taifa nchini Afrika Kusini wakati wa kujiandaa na mchezo dhidi ya Lesotho.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited