Home Soka Tetesi za soka Ulaya leo Jumatano

Tetesi za soka Ulaya leo Jumatano

by Dennis Msotwa
0 comments

Kocha wa Manrochester United Ralf Rangnick amemwambia winga Amad Traore kuwa hayupo kwenye mipango yake hivyo wanataka mkumtoa kwa mopo,PSV ya Uholanzi ndiyo inatajwa kuhitaji saini ya kinda huyo.(Manchester Evening News)

Newcastle ina mpango wa kumgeukia mlinzi wa kati wa Sevilla Diego Carlos baada ya mabingwa wa Ufaransa Lille kugoma kumuuza beki wake Sven Botman kwa dau la paundi milioni 30.(Daily)

Nahodha na mshambuliaji wa Napoli Lorenzo Insigne amekubali kujiunga na Toronto FC inayoshiriki ligi kuu ya Marekani MLS akiwa mchezaji huru pindi mkataba wake na Napoli utakapofikia kikomo mwezi June mwaka huu.(Gazzetta)

banner

Kocha wa Tottenham Antonio Conte amepishana mawazo na mkurugenzi wake wa Ufundi Fabio Paratici kwenye masuala ya usajili.Conte anamtaka kiungo wa Juventus McKenna huku Paratici akimtaka Dejan Kulusevski.(London express)

Mshambuliaji wa Fiorentina Dusan Vlahovic bado hajatupilia mbali wazo la kuongeza mkataba mpya ndani ya klabu hiyo licha ya kuhitajika na vilabu vya Arsenal,Juventus na Bayern Munich.(skysports Italia)

Kiungo wa kati wa Bayern Munich Joshua Kimmich amerjea kwenye mazoezi ya timu hiyo baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa Uviko-19 kwa muda wa miezi miwili.

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited