Shirikisho la soka la Tanzania(Tff) limeamua mchezaji Vicent Andrew Dante kurudi katika klabu yake mara moja baada ya mchezaji huyo kugoma kujiunga na timu hiyo.
Tff imeamua hivyo baada ya kusikiliza pande zote mbili ambapo mchezaji huyo alifungua kesi ya kudai fedha zinazokadiriwa kufikia kiasi cha shilingi milioni 45 huku pia akigomea kujiunga na timu hiyo.
Yanga nao walikata rufaa wakimtaka mchezaji huyo kudai madai yake huku akifata taratibu ikiwemo kurejea mazoezini lakini baada ya shirikisho kusikiliza pande zote ndio liliamua mchezaji huyo kurejea klabuni hapo ili pande hizo mbili ziweze kumalizana kwa amani.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.