Home Soka Tizi la Chama Sio Mchezo

Tizi la Chama Sio Mchezo

by Dennis Msotwa
0 comments

Kiungo wa Simba Clatous Chama leo Jumatatu asubuhi Juni 8, ameanza mazoezi ya peke yake chini ya uangalizi wa Kocha wa Viungo, Adel Zrane baada ya kuchelewa kuanza na wenzake wiki mbili zilizopita.

Chama ambaye amerejea nchini jana kutoka nyumbani kwao Zambia, amechelewa kujiunga na wenzake kutokana na mipaka ya nchi hiyo kufungwa kutokana na mlipuko wa homa ya virusi vya corona.

Benchi la ufundi chini ya kocha, Sven Vandenbroeck limekuwa na utaratibu wa kuwapa mazoezi maalumu wachezaji wanaochelewa kuripoti mazoezini ili kuwaweka fiti kuendana na wenzake.

banner

Wiki iliyopita kiungo Francis Kahata naye alipewa mazoezi kama hayo baada ya kuchelewa kurejea kutoka Kenya sababu ikiwa ni ile ile ya mipaka kufungwa kutokana na corona.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited