Site icon Sports Leo

Watatu Hatihati Yanga sc Vs Al Ahly Fc

Soccer Football - CAF Champions League Final - Second leg - Wydad AC v Al Ahly SC - Mohammed V Stadium, Casablanca, Morocco - June 11, 2023 Al Ahly SC players pose for a team group photo before the match REUTERS/Abdelhak Balhaki

Mastaa watatu wa klabu ya Al Ahly ya nchini Misri wapo hatihati kuivaa Yanga sc katika mchezo wa hatua ya makundi ya klabu bingwa barani Afrika utakaofanyika nchini siku ya Jumamosi Disemba 2 katika uwanja wa Benjamin Mkapa Dar es salaam.

Kwa mujibu wa Afisa Habari wa klabu hiyo Gamal Gabr amesema kuwa mastaa hao ni Taher Mohamed, Antony Modeste na Mahmoud Metwaly wanaweza kuukosa mchezo huo kutokana na kusumbuliwa na majeraha.

Pia Gabr amebainisha kuwa klabu hiyo inaweza kuingia nchini jioni ya leo Novemba 30 tayari kwa mchezo huo ikiwa na kikosi cha wachezaji 25 wakiwemo mastaa Percy Tau na Mohmoud Kahrabah.

Yanga sc inatakiwa kushinda mchezo huo dhidi ya mabingwa hao wa bara la Afrika ili kujitengeneza mazingira mazuri ya kufuzu robo fainali kutokea katika kundi D ambapo mchezo wa mwisho ilikubali kipigo cha 3-0 kutoka kwa CR Belouzdad.

Exit mobile version