Home Soka Winga Teleza Wa As Vita Kutua Yanga

Winga Teleza Wa As Vita Kutua Yanga

by Sports Leo
0 comments

Baada ya usajili wa Bernard Morrison aliyetokea DC Motema Pembe ‘kubamba’, inaelezwa Yanga inamnyemelea mchezaji kutoka klabu ya AS Vita ya huko DR Congo.

Winga Tuisila Kisinda ndiye anayetajwa kutakiwa na mabingwa hao wa kihistoria ukiwa ni mkakati wa kuisuka upya Yanga ya mataji.

Nyota huyo ni miongoni mwa waliopendekezwa na kocha Luc Eymaael katika kuimarisha safu yake ya ushambuliaji.

banner

Kisinda ni mmoja wa wachezaji mahiri wa klabu ya AS Vita. Nyota huyo pia anamudu kucheza nafasi ya mshambuliaji wa kati.

GSM ndio inayoipa jeuri Yanga wakati huu, inaelezwa wametenga kitita cha Tsh Bilioni 1.5 kwa ajili ya usajili huku nyota wanne wa kigeni watasajiliwa ambapo Eymael tayari amewasilisha mapendekezo yake.

Afisa Mhamasishaji wa Yanga Antonio Nugaz amesema katika usajili ujao wako tayari kutumia hata dola laki tano kumnasa mchezaji yeyote aliyependekezwa na Eymael.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited