Home Soka Yanga Sc Yaachana na Moloko,Konkoni

Yanga Sc Yaachana na Moloko,Konkoni

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Yanga sc imeamua kuachana na mastaa wake wawili jesus Moloko na Hafidh Konkoni kutokana na kocha Miguel Gamondi kutoridhishwa na viwango vyao katika kikosi hicho kinachowania ubingwa wa ligi kuu nchini kwa mara ya tatu mfululizo.

Yanga sc imeamua kuachana na Moloko kwa makubaliano ya pande mbili baada ya mchezaji huyo kubakiza mkataba wa miezi sita huku kocha Miguel Gamondi akionyesha kutomhitaji kikosini na Konkoni yeye ametolewa kwa mkopo katika klabu ya Dogan Tûrk Birligi ya Cyprus mpaka mwishoni mwa msimu huu.

Yanga sc kuziba nafasi hizo imewasajili Augustine Okrah sambamba na Joseph Guédé Gnadou ambao wataingizwa kwenye usajili wa Yanga sc na kutimiza idadi ya wachezaji 12 na kigeni ambao wanatakiwa kwa mujibu wa kanuni za bodi ya ligi kuu nchini.

banner

Yanga sc katika msimamo wa ligi kuu nchini ipo nafasi ya pili ikiwa na alama 31 ikiwa imecheza jumla ya michezo 11 ambapo Azam Fc ipo kileleni mwa msimamo ikiwa na alama 33.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited