Home Soka Yanga Yaibamiza Friends Rangers

Yanga Yaibamiza Friends Rangers

by Sports Leo
0 comments

Yanga sc imeibuka na ushindi wa magoli mawili dhidi ya Friends Rangers katika mechi ya kirafiki iliyopigwa asubuhi ya leo mjini Morogoro katika kambi ya timu hiyo iliyopo chuo cha biblia kilichopo Bigwa mjini humo.

Mabao ya Yanga yalifungwa na Sidney Urikhob dakika ya 38 bao lililodumu hadi mapumziko na kipindi cha pili iliwachukua yanga dakika 23 kupata bao la pili mfungaji akiwa ni nahodha mpya wa klabu hiyo Papy Kabamba Tshitshimbi mabao yaliyodumu mpaka mwisho wa mchezo.

Yanga imekua inaibuka na ushindi katika mchezo yote ya kirafiki ambao imecheza mpaka sasa huku ikifunga magoli zaidi ya 20 na kufungwa magoli chini ya matatu hali inayoonyesha uimara wa safu za ulinzi na ushambuliaji.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited