Home Soka Yanga Yaibamiza Mwadui

Yanga Yaibamiza Mwadui

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Yanga sc imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mwadui Fc mchezo wa Ligi Kuu nchini Tanzania bara uliochezwa katika uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.

Bao la Yanga lilifungwa dakika ya 6 na Balama Mapinduzi kufuatia shambulizi la kushtukiza lililoanzia kwa Haruna Niyonzima kisha Jafar Mohamed aliyepiga krosi ambapo Ditram Nchimbi alikosa goli baada ya Kipa kucheza kisha mpira kumkuta Mfungaji.

Bao hilo limeweka rekodi ya kuwa bao la kwanza nchini katika mashindano rasmi tangu ligi isimamishwe siku 95 zilizopita kufuatia kusambaa kwa Virusi vya ugonjwa wa homa ya Mapafu (Covid-19).

banner

Ushindi huo Yanga imesaalia nafasi ya tatu ikiwa na pointi 54 sawa na klabu ya Azam fc japo wanatofautiana kwa tofauti ya mabao ya kushinda na kufungwa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited