Uongozi wa klabu Yanga umesema hauna mpango wa kumuacha beki wao kisiki Lamine Moro ambaye aliandika barua ya kuvunja mkataba wake kutokana na madai ya mishahara
Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo, Mwenyekiti wa Yanga Dk Mshindo Msolla amekiri beki huyo kuwa na madai ya mishahara miwili na sio mitatu
“Lamine bado ni mchezaji wetu kwani ana mkataba wa mwaka mmoja na nusu. Madai yake ya mishahara ya miezi miwili pamoja na wachezaji wengine wote watalipwa leo,” amesema
Ataja sababu ya kumtema Sadney
Aidha Dk Msolla amesema uongozi umeamua kuachana na aliyekuwa mshambuliaji wake Sadney Urikhob kutokana na uwezo wake kutoendana na matarajio ya klabu
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Dk Msolla amesema Sadney aliomba mkataba wake kuvunjwa na uongozi uliridhia kwa kuwa hakuweza kufikia matarajio ya timu
“Tumemwachia Sadney kwakuwa uwezo wake ni mdogo lakini tunapambana kumzuia Lamine Moro asiondoke. Mpira ni mchezo wa wazi , uwezo wa beki huyu kila mtu ameuona”
Habari kwa msaada wa Mitandao ya Kijamii