Home Soka Yanga Yamkosa Niyonzima

Yanga Yamkosa Niyonzima

by Sports Leo
0 comments

Sasa ni rasmi klabu ya Yanga imemkosa kiungo mkabaji raia wa Rwanda Ally Niyonzima baada ya kiungo huyo kuamua kusaini mkataba wa miaka miwili katika klabu ya Kiyovu Stars inayoshiriki ligi kuu nchini humo.

Kiungo huyo alikua akiwania na klabu ya Yanga ikiwa ni mapendekezo ya benchi la ufundi chini ya mkufunzi Luc Eymael aliyetaka awepo mbadala ya nahodha Papy Tshitshimbi kikosini humo.

Ally Niyonzima mwenye uwezo mzuri wa kucheza nafasi ya kiungo mkabajiamefikia muafaka huo baada ya kutopata muafaka wake mapema wa kujiunga na Yanga ambapo aliambiwa asubiri mpaka finali ya kombe la shirikisho FA ndiyo atalipwa malipo yake ya awali ( advance).

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited