Home Soka Yanga Yaweka Rekodi Taifa

Yanga Yaweka Rekodi Taifa

by Dennis Msotwa
0 comments

Mechi ya watani wa jadi Yanga vs Simba iliyochezwa Jumapili Machi 8, 2020 imevunja rekodi ya mapato kwa kuiingizia serikali shilingi milioni 153.2 kiasi ambacho hakijawahi kupatikana katika historia ya mechi za watani hao.

Taarifa hiyo imetolewa mapema leo na Msemaji wa Serikali Dkt. Hassan Abbas wakati akiongea na vyombo vya habari mjini Dodoma.

Aidha ukiondoa mapato ya Serikali, jumla ya Tsh Milioni 545.4 zilikuwa ni mapato ya timu (Yanga) ambao walikuwa wenyeji wa mchezo huo uliofanyika machi 8 mwaka huu.

Hii ni rekodi mpya katika historia ya uwanja huo uliozinduliwa mwaka 2007 ukilinganisha na mechi zingine zilizochezwa uwanja hapo zikiwemo za kimataifa.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited