Home Soka Zahera Apewa Mechi 3 Yanga

Zahera Apewa Mechi 3 Yanga

by Sports Leo
0 comments

Kuna taarifa za chinichini zinadai klabu ya Yanga sc imempa mechi tatu kocha Mwinyi Zahera ili kuamua hatima yake endapo atashindwa kuipatia ushindi timu hiyo katika mechi hizo.

Taarifa hizo zinadai uongozi wa Yanga umeamua kumpa mechi hizo kocha huyo baada ya kutofurahishwa na matokeo ya mechi ya kwanza ya ligi dhidi ya Ruvu shooting ambapo timu hiyo ilipoteza kwa bao moja licha ya kupata nafasi kadhaa za kufunga.

“Sisi kama viongozi hatuna hizo taarifa kwamba tumempa mechi 3 kocha wetu Zahera Mwinyi asiposhinda mechi tatu tunamtimua”-Rodgers Gumbo, Mwenyekiti Kamati ya Mashindano

banner

Licha ya uongozi wa klabu hiyo kukana suala hilo lakini taarifa za ndani zinadai mpango huo upo japo hauna nguvu sana lakini mashabiki wa timu hiyo hawaoneshi kufurahishwa na matokeo ya timu hiyo licha ya kufanya usajili wa nguvu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited