Home Soka Zahera Arejea Kufuata Manoti

Zahera Arejea Kufuata Manoti

by Sports Leo
0 comments

Kocha msaidizi wa timu ya taifa ya Kongo Mwinyi Zahera amerejea nchini kufuatilia stahiki zake katika klabu ya Yanga baada ya timu hiyo kuvunja mkataba na kocha huyo.

Zahera alivunjiwa mkataba na klabu hiyo ukiwa umebakiza zaidi ya miezi sita ili kufikia tamati baada ya kuwa na mwenendo usioridhisha katika klabu hiyo.

Kocha huyo baada ya kuvunjiwa mkataba aliondoka nchini kujiunga na timu ya taifa na baada ya kumaliza majukumu amerejea nchini ili kuchukua stahiki zake ambazo ni zaidi ya shilingi milioni hamsini za kitanzania ikiwa ni majumuisho ya pesa ya kuvunjia mkataba na madeni ya mishahara iliyopita.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited