Home Makala Yanga sc Wamwalika Samia kwa Mkapa

Yanga sc Wamwalika Samia kwa Mkapa

by Sports Leo
0 comments

Uongozi wa Yanga SC umemualika Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan kushuhudia mchezo wao wa ligi kuu dhidi ya KMC katika kilele cha Mwaka mmoja wa Urais wake siku ya jumamosi kwenye uwanja wa Mkapa.
Akizungumza mbele ya waandishi wa habari Afisa habari wa klabu hiyo Haji Manara amesema kuwa wamwemwalika mkuu huyo wa nchi kushuhudia mchezo huo ikiwa ni ishara ya kushikamana na Serikali katika kuadhimisha mwaka mmoja wa Rais Samia madarakani baada ya kufariki kwa Hayati John Magufuri.
“Tumemuomba Rais Samia kama ratiba yake haitambana basi awe mgeni rasmi katika mechi yetu na KMC” alisema Haji Manara
Pia Msemaji huyo wa klabu hiyo aliyahamia akitokea Simba sc Haji Manara amesema kuwa mashabiki wa klabu hiyo wataanza kwa kuchangia damu hospitali ya Muhimbili siku ya Ijumaa march 18 ambapo wanayanga 200 wa kwanza kuwahi kuchangia damu watapata zawadi ya jezi bure.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited