Home Soka Saido Hatarini Kusepa Yanga sc

Saido Hatarini Kusepa Yanga sc

by Dennis Msotwa
0 comments

Mkataba wa kiungo mshambuliaji wa klabu ya Yanga sc Saido Ntibanzokiza umebakisha siku 39 kutamatika huku klabu hiyo ikiwa bado na mechi kadhaa za ligi kuu kabla ya msimu kuisha.

Ntibanzokiza licha ya mkataba wake kuelekea kuisha ameibuka kama mchezaji muhimu katika kikosi cha Yanga sc ambapo mpaka sasa amefunga jumla ya mabao 6 na kutoa usaidizi wa mabao kadhaa klabuni hapo akichuana kwa ukaribu na Fiston Mayele mwenye mabao 11 ya ligi kuu nchini.

Saido alijiunga na Yanga sc kwa mkataba wa mwaka mmoja na nusu baada ya kuonekana katika mchezo kati ya Tanzania na Burundi aliwahangaisha viungo wa Stars akiwemo Jonas Mkude ambaye alipewa kadi nyekundu katika mchezo huo.

banner

Mchezaji huyo ni kati ya mastaa ambao mikataba yao inaisha msimu huu klabuni hapo japo wa kwake utaisha huku ikiwa ligi kuu haijaisha na tayari Mtendaji mkuu wa klabu ya Yanga sc Senzo Mazingisa amesisitiza kuwa suala hilo lipo mikononi mwa kocha Nasredine Nabi akisubiriwa kutoa ruhusu ili mchezaji huyo aongeze mkataba.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited