Home Soka Saido,Yacouba Kuwakosa Namungo Fc

Saido,Yacouba Kuwakosa Namungo Fc

by Sports Leo
0 comments

Pamoja na kwamba amebakisha chini ya siku arobaini amalize mkataba wake na klabu ya Yanga sc mchezaji Saido Ntibanzokiza ataukosa mchezo wa ligi kuu dhidi ya Namungo Fc kutokana na kusumbuliwa na majeraha.

Mchezaji huyo ameibuka kuwa mmoja ya wachezaji muhimu katika klabu yake akifunga mabao 6 nyuma ya kinara Fiston Mayele amekua akisumbuliwa na majeraha madogo madogo yanayomfanya akose baadhi ya michezo ikiwemo huu dhidi ya Namungo Fc ambao Yanga sc wanahitaji alama tatu muhimu.

Yanga sc wakishinda mchezo huo wataongeza pengo la alama mpaka 13 dhidi ya hasimu wake Simba sc kutoka kumi za hivi sasa huku wakijiandaa kuvaana wao kwa wao April 30.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited