Home Soka Yanga sc Yamnyatia Beki Angola

Yanga sc Yamnyatia Beki Angola

by Sports Leo
0 comments

Inaripotiwa kuwa Mabosi wa Yanga wameanza kumnyatia beki wa kushoto wa kimataifa wa DR Congo, Lomalisa Mutambala anayecheza soka la kulipwa nchini Angola katika timu ya Sagrada Esperanca aliyokua anaichezea Carlos Calinhosi ambaye alikua kiungo mshambuliaji wa zamani wa klabu hiyo.

Klabu hiyo itakua na nafasi nzuri ya kumsajili beki huyo ikizingatiwa  kuna uhusiano mzuri kati ya vigogo wa Yanga na Sagrada baada ya awali kukamilisha dili la Carlinhos kuja Jangwani japo hakua na maisha mazuri klabuni hapo.

Beki huyo anakuja kuongeza nguvu upande wa kushoto ambako imemlazimu kocha Nasredine Nabi kumhamishia Kibwana Shomari baada ya Yassin Mustapha na David Bryson kushindwa kuonyesha makali eneo hilo huku majeraha ya mara kwa mara yakisababisha viwango vyao kutokua imara.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited