Home Makala Aziz Ki Aitwa B/Faso

Aziz Ki Aitwa B/Faso

by Sports Leo
0 comments

Staa wa klabu ya Yanga sc Stephane Aziz Ki ameitwa katika kikosi cha timu yake ya Taifa ya Burkina Faso kinachojiandaa na michezo miwili ya kimataifa yakalenda ya shirikisho la soka duniani (Fifa) dhidi ya Togo.

Aziz Ki aliyejiunga na klabu ya Yanga sc msimu huu alianza kwa kuchechemea katika ligi kuu nchini kutokana na kutozoea mazingira lakini kadri siku zinavyokwenda amefanikiwa kuonyesha kipaji cha hali ya juu sambamba na kufunga magoli muhimu kwa klabu hiyo.

Moja ya mabao yatakayokumbukwa na mashabiki wa soka hasa nchini ni lile dhidi ya Club Africain nchini Tunisia ambapo aliunganisha kwa shuti kali pasi ya kichwa na Fiston Mayele na kuiwezesha Yanga sc kufuzu hatua ya makundi ya michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika.

banner

Aziz Ki anatarajiwa kujiunga na timu yake ya taifa hivi karibuni baada ya kumaliza mechi za kombe la shirikisho na ile ya kimataifa dhidi ya Real Bamako inayotarajiwa kufanyika machi nane mwaka huu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited