Home Makala Okwi,Aucho Ndani ya The Cranes

Okwi,Aucho Ndani ya The Cranes

by Sports Leo
0 comments

Kiungo wa Yanga, Khalid Aucho na mshambuliaji Emmanuel Okwi ni miongo mwa wachezaji 30 walioitwa kwenye kikosi cha Timu ya Taifa ya Uganda kitakachoingia kambini hivi karibuni kwa ajili ya maandalizi ya kumenyana na Taifa Stars katika kuwania kufuzu michuano ya Afcon 2023.

Okwi mwenye umri wa miaka 30 kwa sasa ni mchezaji wa zamani wa Sc Club Villa,Simba sc na Yanga sc za nchini Tanzania aliondoka nchini mwaka 2019 na kujiunga na klabu ya Al Ittihad inayoshiriki ligi kuu nchini Misri ameitwa na kocha Milutin Sredojević maarufu kama “Micho” kama mshambuliaji huku kiungo wa Yanga sc Khalid Aucho akiitwa kama kiungo mwandamizi.

Aucho amekua na wakati mzuri tangu ajiunge na klabu ya Yanga sc akiwa na uhakika wa kucheza katika kikosi cha kwanza na kufanikiwa kushinda mataji kadhaa ya ligi kuu,ngao ya jamii na kombe la shirikisho la Azamsports huku hivi sasa akishiriki katika michuano ya kombe la shirikisho la Caf.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited