Home Soka Watatu Hatihati Yanga sc Vs Al Ahly Fc

Watatu Hatihati Yanga sc Vs Al Ahly Fc

by Dennis Msotwa
0 comments

Mastaa watatu wa klabu ya Al Ahly ya nchini Misri wapo hatihati kuivaa Yanga sc katika mchezo wa hatua ya makundi ya klabu bingwa barani Afrika utakaofanyika nchini siku ya Jumamosi Disemba 2 katika uwanja wa Benjamin Mkapa Dar es salaam.

Kwa mujibu wa Afisa Habari wa klabu hiyo Gamal Gabr amesema kuwa mastaa hao ni Taher Mohamed, Antony Modeste na Mahmoud Metwaly wanaweza kuukosa mchezo huo kutokana na kusumbuliwa na majeraha.

Pia Gabr amebainisha kuwa klabu hiyo inaweza kuingia nchini jioni ya leo Novemba 30 tayari kwa mchezo huo ikiwa na kikosi cha wachezaji 25 wakiwemo mastaa Percy Tau na Mohmoud Kahrabah.

banner

Yanga sc inatakiwa kushinda mchezo huo dhidi ya mabingwa hao wa bara la Afrika ili kujitengeneza mazingira mazuri ya kufuzu robo fainali kutokea katika kundi D ambapo mchezo wa mwisho ilikubali kipigo cha 3-0 kutoka kwa CR Belouzdad.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited