Home Makala Simba Sc,Chama Mambo Safi

Simba Sc,Chama Mambo Safi

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc imeamua kumsamehe kiungo wake Cletous Chama baada ya kumsimamisha kwa muda kutokana na tatizo la utovu wa nidhamu ambalo lilitokea mwaka jana kuelekea mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Wydad Athletic Club uliofanyika katika uwanja wa Benjamini Mkapa Dar es salaam.

Inadaiwa kuwa kiungo huyo alimtolea lugha chafu kocha msaidizi wa klabu hiyo wakati wa mazoezi ya kupasha mwili kuelekea mchezo huo ambapo taarifa kutoka klabuni hapo ilisema kuwa klabu hiyo imemsimamisha mchezaji huyo na kumpeleka kamati ya nidhamu ya klabu hiyo.

banner

Leo klabu hiyo imetoa taarifa iliyopokelewa kwa maoni tofauti ambapo klabu hiyo imeamua kumsamehe mchezaji huyo baada ya kuomba radhi tayari amesafiri kuelekea mkoani Kigoma kujiandaa na mchezo dhidi ya Mashujaa Fc utakaofanyika kesho katika uwanja wa Lake Tanganyika.

Mkataba wa Chama na Simba sc unatarajiwa kufika tamati mwishoni mwa msimu huu ambapo taarifa zinadai kuwa mabosi wa klabu hiyo wana mpango wa kuachana naye hasa wakipata mbadala sahihi wa nafasi yake klabuni hapo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited