Home Soka Kyombo Atua Rasmi Mamelod Sundowns

Kyombo Atua Rasmi Mamelod Sundowns

by Dennis Msotwa
0 comments

Mshambuliaji wa Timu ya Taifa ya vijana ya Tanzania Habib Kyombo amekamilisha rasmi uhamisho wa kujiunga wa timu ya Mamelod Sundowns inayoshiriki ligi kuu ya Afrika kusini kwa mkataba wa miaka minne.

Kyombo 19 alifahamika katika ramani ya soka alipokua anaichezea timu ya Mbao Fc ya mwanza na baadae akajiunga na Singida United na kupata nafasi ya kufanya majaribio katika timu hiyo ambapo alifuzu lakini alishindwa kukamilisha usajili mpaka dirisha la usajili lilipofunguliwa rasmi.

Katika barua aliyoiandika mchezaji huyo katika mtandao wake wa kijamii alithibitisha kukamilisha usajili na kuwashukuru watu mbalimbali ikiwemo timu yake ya zamani ya Singida united na kampuni iliyomsaidia kukamilisha usajili ya Shadaka sports managements.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited