Home Makala Kaizer Chiefs Yakomaa na Diarra

Kaizer Chiefs Yakomaa na Diarra

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Kaizer Chief ya Afrika Kusini Imefungua mlango wa mazungumzo na Uongozi wa klabu ya Yanga sc ya Tanzania kuona kama wanaweza kumpata Mlinda lango huyo bora kwenye dirisha kubwa la usajili.

Kaizer chiefs hawajaridhishwa na ubora wa magolikipa wao wawili raia wa Rwanda Fiacre Ntwari na Raia wa Afrika kusini Bruce Bvuma walioruhusu mabao 24 kwenye michezo 20 ya ligi kuu.

Kocha Nasredine Mohamed Nabi anataka kuhakikisha kuwa kikosi chake kinapambana kumpata golikipa huyo mzoefu wa soka barani Afrika ambapo mpaka sasa Pamoja na klabu hiyo kutuma ofa bado haijajibiwa na klabu yake ya Yanga Sc.

banner

Diarra mwishoni mwa msimu uliopita aliongeza mkataba wa miaka mitatu na klabu yake ya Yanga sc kuendelea kuitumikia klabu hiyo hivyo Kaizer Chiefs inapaswa kutoa fedha ndefu kumnasa kipa huyo aliyetokea kuwa kipenzi cha mashabiki wa klabu hiyo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited