Home Soka Kindoki Kurudi Kongo

Kindoki Kurudi Kongo

by Dennis Msotwa
0 comments

Kocha wa timu ya Yanga sc Mkongomani Mwinyi Zahera ameweka bayani kuwa usajili wa mshambuliaji mpya wa klabu hiyo aliyetua jana usiku atachukua nafsi ya kipa Klaus Nkizi Kindoki atakayerudishwa Fc Lupopo.

Kocha huyo amesema kuwa Kindoki atarudishwa Kongo ili kutoa nafasi ya usajili wa David Molinga(Falcao) ili kukidhi hitaji la wachezaji kumi wa kigeni kama kanuni zinavyotaka.

“Mchezaji huyu ametokea Kongo kwenye timu waliyotokea Makambo na Kindoki na tulishafanya mazungumzo na Kindoki kuwa atarudi kule Lupopo akaive sawasawa hivyo hakuna utata kila kitu kipo sawa”Alisema Zahera.

banner

Kuondoka kwa kipa huyo klabuni kunamaanisha timu hiyo itabaki na makipa watatu,Mkenya Farouk Shikalo na wazawa Metacha Mnata na Ramadhani Kabwili.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited