Home Soka Yondani Arejea Kishingo Upande

Yondani Arejea Kishingo Upande

by Sports Leo
0 comments

Beki kisiki wa Yanga sc Kelvin Yondani amerejea klabuni hapo na kujiunga na kambi ya mazoezi ya klabu hiyo huku akisisitiza kumaliziwa stahiki zake zote anazoidai klabu hiyo.

Inasemekana beki huyo alikubali kuzungumza na baadhi ya viongozi wa klabu hiyo na kufikia makubaliano ya kumaliza tofauti hizo huku akiahidiwa kuwa madai yake yatashughulikiwa huku akiwa kambini na timu hiyo kujiandaa na mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Township Rollers ugenini nchini Botswana.

Yondani na wenzake Juma Abdul na Andrew Vicent wanadaiwa kugoma ili kushinikiza uongozi kuwalipa madai yao ya fedha za usajili wanazodai baada ya klabu hiyo kusajili wachezaji wapya na kuwalipa fedha zao zote ilihali wao wakiendelea kusubiri tangu fedha za mwaka jana.

banner

Awali kocha Mwinyi Zahera alisisitiza beki huyo ana ruhusa maalumu hivyo atajiunga na timu hiyo hivi karibuni huku akiweka bayana kuhusu mgomo wa Juma Abdul na Andrew Vicent kuwa wana madai ya msingi hivyo wanapaswa kusikilizwa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited