Home Soka Goti Lamtibulia Beki Yanga

Goti Lamtibulia Beki Yanga

by Dennis Msotwa
0 comments

Maumivu ya goti aliyoyapata beki wa Yanga Ally Ally yamemfanya atolewe kwenye kikosi cha timu hiyo kitakachovaana na Township Rollers jijini Gaborone Botswana.

Beki huyo mfupi mwenye uimara katika kucheza mipira ya juu alisajiliwa na Yanga akitokea Kmc ya jijini Dar es salaam na amefanikiwa kupata nafasi katika baadhi ya michezo ukiwemo dhidi ya Rollers alipoingia kuchukua nafasi ya Paulo Godfrey ambaye alipata majeraha.

Beki huyo alikuwemo kwenye msafara wa wachezaji waliosafiri kwenda nchini humo japo kutokana na maumivu hayo kuna uwezekano wa kutocheza mchezo huo.a

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited